Sunday 15 June 2014

Published 04:24 by with 0 comment

Unyama Mwingine: Hausigeli ( binti wa kazi )Ajeruhiwa vibaya na bosi wake na kulazwa Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar


http://1.bp.blogspot.com/-mGUaEBsOAiU/U5plXCYk3bI/AAAAAAAAIG8/OcdgZzjMGDY/s1600/mwananyamala.jpg

Hausigeli aitwaye Melina Mathayo mwenye umri kati ya miaka 15, ameumizwa vibaya sehemu za kichwani na kulazwa katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam baada ya kupigwa na bosi wake aitwaye Yasintha Rwechungura mkazi wa Boko.

Akiongea na mwanahabari wetu akiwa katika hospitali hiyo, Melina amesema amekuwa akipigwa na bosi wake huyo mara kwa mara kwa kutumia waya, brenda na vifaa vingine japo alikuwa akiogopa kusema.

Vitendo hivi vya ukatili vinaonekana kushamiri kwa sasa ikiwa ni siku chache baada ya hausigeli aitwaye Yusta kuripotiwa kung'atwa na bosi wake aitwaye Amina Maige aliyepandishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni.
  
Binti huyo aliyeletwa Mwananyamala jana alfajiri akiwa na hali mbaya amefanya kazi kwa miaka miwili nyumbani kwa mama huyo mwenyeji wa mkoani Kagera.
  
http://4.bp.blogspot.com/-rfWS4yH1k8g/U5pu_otTR-I/AAAAAAAAIHc/5N1r1j8el9I/s1600/mateso.jpg
Melina alikuwa akiongea na mwanahabari wetu akiwa na mpira wa kuongezewa damu mwilini na amehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala amethibitisha kutokea tukio hilo.

      edit

0 comments:

Post a Comment