Akiongea na Global TV, Flora Mbasha
amezungumzia tuhuma hizo na kuelezea kuwa kabla ya kufanya tukio hilo alikuwa
hamuelewi kabisa mume wake ambaye Jumapili alimbadilikia kutoka na kile
anachosema walikuwa wametofautiana na ndipo mumewe akafikia hatua ya kumkaba na
kumtishia kumuua.
“Kabla sijatoka ndani alisema ‘we leo
lazima nikufundisha adabu’, alinishika akaniniga yaani mpaka akaniachia maalama
kwenye shingo yani hivi ninavyozungumza mpaka sasa hivi bado shingo yangu
inaniuma hata kuongea siwezi.”
Mwimbaji huyo anadai kuwa mume wake
hakuwa katika hali ya kawaida na baada yakumkataza asichukue gari Flora,
mchungaji Gwajima alimpigia simu na kisha kumtumia gari afike kanisani na
watoto aliokuwa amemwambia awapeleke.
Hata hivyo hatua hiyo ilimchafua zaidi Emmanuel ambaye alipiga simu na kutukana matusi muda mrefu tena matusi ya nguoni.
Ameeleza kuwa siku hiyo hakurudi
nyumbani na siku iliyofuata ndipo binti huyo amedai sio mdogo wake bali
walikuwa wanaishi nae alimpigia simu ndugu yake Flora na kumpa mkasa wa kubakwa
na kusababishiwa maumivu na bwana Mbasha.
“Huo usiku sikurudi nyumbani na asubuhi
Jumatatu yule binti akapiga simu, hakunipigia mimi akampigia mdogo wangu
mwingine akamwambia mimi naondoka mimi shemeji ameninyanyasa amenidhalilisha
kanifanyia kitendo kibaya sana, sasa akamuuliza amekufanyia nini?
"Akawa hawezi kuongea kwenye simu akamshauri tu kwamba usiondoke subiri dada yako atakapokuja kwanza anarudi muda si mrefu…Kwa sababu yule binti tulikuwa tunakaa nae nyumbani namtunza mimi.
"Kwa hiyo nilikuwa naishi nae hapo ndani kwa hiyo alikuwa kama ni mtoto wa kwangu mimi tulikuwa tunamlea pamoja na mme wangu.”
Hadi sasa bado mume wa Flora
hajapatikana na polisi wanaendelea na uchunguzi wa tuhuma hizo za ubakaji.
Tazama video ya mahojiano hayo hapo chini.
0 comments:
Post a Comment